"Regina caeli" (tamka: reˈdʒina ˈtʃeli; maana yake Malkia wa Mbingu)ni antifona inayotumika kumuelekea Bikira Maria katika Kanisa la Kilatini wakati wa Pasaka, kuanzia Dominika ya Ufufuko wa Yesu hadi Pentekoste.
Katika siku hizo hamsini ndiyo antifona pekee inayotumika kumalizia Sala ya mwisho ya Liturujia ya Vipindi [2] lakini pia inashika nafasi ya sala ya Angelus (inayofanyika mara tatu kwa siku: asubuhi, adhuhuri na jioni).
Mtunzi wa Regina caeli hajulikani. Kimaandishi inapatikana katika kitabu cha antifona cha mwaka 1200 hivi kinachotunzwa katika Basilika la Mt. Petro, huko Vatikani, jijini Roma.[5]