Mt. Hilda katika kioo cha rangi, kanisa kuu la Gloucester Cathedral.
Maghofu ya Abasia ya Whitby.

Hilda wa Whitby (614 hivi – 17 Novemba 680) alikuwa abesi mwanzilishi[1][2] wa monasteri ya Whitby, iliyofuata desturi za Ukristo wa Kiselti. Ndipo palipofanyika Sinodi ya Whitby[3]iliyokubali kufuata desturi za Kanisa la Roma.

Muhimu katika kuvuta Waangli na Wasaksoni katika Ukristo, alisimamia pia monasteri nyingine kwa hekima yake maarufu.

Habari za Hilda zinategemea hasa kitabu cha historia ya Kanisa kilichoandikwa na Beda Mheshimiwa mwaka 731.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waanglikana kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake au siku nyingine.

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi

[hariri | hariri chanzo]
  1. "Hilda of Whitby / Hild of Streonshalh 614-680 Educator of Women". Iliwekwa mnamo 21 Machi 2016.((cite web)): CS1 maint: date auto-translated (link)
  2. Thurston, Herbert. "St. Hilda." The Catholic Encyclopedia. Vol. 7. New York: Robert Appleton Company, 1910. 7 May 2013
  3. "St. Hilda", Parish Church of St. Wilfrid, Bognor

Vyanzo

[hariri | hariri chanzo]

Marejeo mengine

[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.