Halley alizaliwa katika kaunti ya Middlesex, Uingereza. Babake Edmond Halley alikuwa fundi wa sabuni mjini London na tajiri. Aliposoma shuleni kijana Halley alivutwa sana na hisabati. Alisoma shule ya St Paul's alipoanza kujifunza astronomia. 1673 aliingia Queen's College mjini Oxford. Wakati bado alikuwa mwanafunzi, Halley alitunga makala kuhusu Mfumo wa Jua na madoa ya Jua.
Pale Oxford Halley alifahamiana na mwanaastronomia mashuhuri John Flamsteed aliyekuwa akikusanya habari za nyota zote zilizoweza kutazamiwa kwenye angakaskazi na kuandaa orodha ya namba za Flamsteed. Halley alijitolea kufanya kazi ileile kwa ajili ya angakusi.
Mnamo mwaka 1676, alipokuwa na umri wa miaka 20, aliondoka katika Oxford akasafiri kwenda kisiwa cha St Helena katika Atlantiki ya kusini akaanzisha paoneaanga na kuchunguza nyota akaweza kuorodhesha nyota 341 za angakusi. [2] Mafanikio haya yalimpatia shahada ya uzamili (MA).
Kwenye Septemba 1682 alitazama nyota yenye mendo kwenye aliyotambua kuwa ni nyotamkia ailiyowahi kutazamiwa. Alitabiri kurudi kwake mnamo mwaka 1758. Halley mwenyewe aliaga dunia kabla ya marudio lakini wataalamu wa wakati walikumbuka utabiri wake n hivyo nyotamkia hii iliyoendelea kurudi ilipata jina lake.
Mnamo 1686, Halley alichapisha sehemu ya pili ya matokeo kutoka kwa msafara wake wa St. Helena . Hii ilikuwa makala kuhusu upepo na monsuni. Hapa alitambua ni joto la Jua linalosababisha miendo katika angahewa. Aliatambua uhusiano baina kanieneo angahewa jinsi inavyopinwa kwa barometa na kimo juu ya usawa wa bahari . Halley pia alimshawishi Sir Isaac Newton kuchapisha kitabu kuhusu uvumbuzi wake wa graviti .