Sanamu ya Mt. Helena, Musei Capitolini, Roma, Italia.

Helena (kwa Kigiriki: Ἑλένη, Helénē; kwa Kilatini: Flavia Iulia Helena Augusta; 246/248 – Roma, 330 hivi) alikuwa mke wa kaisari Constantius Chlorus.

Alijitokeza kwa bidii zake za kusaidia fukara; pia alikuwa anaingia makanisani kwa moyo wa ibada akijichanganya na umati wa waumini [1].

Alipohiji Yerusalemu ili kuheshimu mahali pa kuzaliwa, kuteseka na kufufuka Yesu Kristo, alitembelea pango na msalaba wake akapajengea mabasilika ya fahari [2].

Ni maarufu hasa kama mama wa Konstantino Mkuu aliyemuelekeza kupenda Ukristo na hivyo alichangia uanzishaji wa uhuru wa dini katika Dola la Roma baada ya miaka 250 ya dhuluma dhidi yake.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 18 Agosti[3] au 21 Mei.

Tazama pia

Tanbihi

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/66500
  2. https://www.santiebeati.it/dettaglio/66500
  3. Martyrologium Romanum

Vyanzo

Marejeo mengine

Viungo vya nje

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Helena of Constantinople
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.