Bendera ya Afrika Kusini
Bendera ya Afrika Kusini 1928-1994
Bendera ya Afrika Kusini 1910-1928

Bendera ya Afrika Kusini ni ya pekee kati ya bendera za dunia ikiwa na rangi sita.

Kimsingi muundo wake ni milia mitatu ya kulala ya nyekundu, kijani na buluu; pamoja na kanda nyembamba nyeupe juu na chini ya mlia wa kijani.

Huu mlia wa katikati (kijani pamoja na kanda neupe) unagawiwa ukionyesha umbo la "Y" ya kulala. Pembetatu ndani ya kichwa cha "Y" ina rangi nyeusi inayotengwa na ijani ya "Y" kwa kanda nyembamba ya dhahabu.

Bendera ilikubaliwa Aprili 1994 baada ya mwisho wa utawala wa ubaguzi wa mbari. Ilitengenezwa na Frederick G. Brownell kama bendera ya muda kwa ajili ya uchaguzi wa Aprili 1994 na kuapishwa kwa Nelson Mandela kama rais wa Afrika Kusini tarehe 10. 05. 1994. Imependwa na watu na kupokelewa katika katiba kama bendera ya kudumu.

Kati ya rangi ni zile za Ethiopia au rangi za Umoja wa Afrika: kijani - njano (=dhahabu) na nyekundu. Bendera inaendeleza pia rangi za bendera ya zamani ya Afrika Kusini iliyotumiwa hadi 1994 yaani machungwa (=dhahabu), nyeupe na buluu.

Vilevile rangi za bendera ya ANC zimepatikana: nyeusi, kijani na njano.

Hakuna maelezo rasmi juu ya maana ya rangi hizi. Lakini mtungaji wa bendera Brownell alieleza mawazo yake wakati wa kutunga hivyo:

Viungo vya Nje

[hariri | hariri chanzo]