Picha takatifu ya Mt. Simeoni huko Sanok, Polandi.

Simeoni wa Mnarani (kwa Kisiria: ܫܡܥܘܢ ܕܐܣܛܘܢܐ, šamʻun dasṯonáyá, kwa Kigiriki: Συμεών ὁ στυλίτης, Symeón o Stylítis; kwa Kiarabu سمعان العمودي, Simʿān al-ʿAmūdī; kwa Kiingereza: Symeon the Stylite; Sis (leo nchini Uturuki), 390 hivi - Qalaat Semaan, Syria, 2 Septemba 459[1][2]) alikuwa mkaapweke kutoka Assyria aliyepata umaarufu kwa kuishi kiadilifu sana miaka 37 juu ya mnara karibu na Aleppo[3][4][5][6].

Pengine anaongezewa sifa "mzee" ili kumtofautisha na waliofuata mtindo wake huo kama Simeoni wa Mnarani Kijana, Simeoni wa Mnarani III na Simeoni wa Mnarani wa Lesbos.

Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi, Waorthodoksi wa Mashariki, Wakatoliki na Waanglikana kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 27 Julai[7], 5 Januari, 1 Septemba au nyingine kadiri ya madhehebu.

Tazama pia

Tanbihi

  1. "Saint Simeon Stylites", Encyclopedia Britannica
  2. "Saint Simeon Stylites", New Advent Catholic Encyclopedia
  3. "Saint Simeon Stylites", Encyclopedia Britannica
  4. "Saint Simeon Stylites", New Advent Catholic Encyclopedia
  5. Boner, C. (Summer 2008). "Saint Simeon the Stylite". Sophia. 38 (3). The Eparchy of Newton for the Melkite Greek Catholics: 32. ISSN 0194-7958. ((cite journal)): Cite has empty unknown parameter: |coauthors= (help)CS1 maint: date auto-translated (link)
  6. https://www.santiebeati.it/dettaglio/64600
  7. Martyrologium Romanum

Marejeo

Viungo vya nje

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Simeoni wa Mnarani
Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.