Youth career | |||
---|---|---|---|
2004–2005 | 1860 Munich | ||
2005–2007 | Brescia | ||
Senior career* | |||
Miaka | Timu | Apps† | (Gls)† |
2007–2009 | Brescia | 22 | (3) |
2009 | West Ham United | 10 | (0) |
2009– | Fiorentina | 0 | (0) |
Timu ya Taifa ya Kandanda‡ | |||
2008– | Germany U19 | 11 | (4) |
2008– | Germany U20 | 2 | (0) |
* Senior club appearances and goals counted for the domestic league only and correct as of 19 May 2009 (UTC). † Appearances (Goals). |
Savio Nsereko (anajulikana kama Savio[1]; amezaliwa Kampala, Uganda, 27 Julai, 1989) ni mchezaji wa mpira wa miguu; anaweza kucheza kama mshambuliaji au winga lakini huelekea kucheza mrengo wa kushoto, ili aweze kukata ndani ya ulinzi na kupiga mkwaju na mguu wake wa kulia.
Nsereko alizaliwa mjini Kampala na alianza kazi yake katika 1860 Munich. Aliingia Brescia katika majira ya joto ya 2005,akiwa na umri wa 16, umri wa chini ulioruhusiwa na FIFA katika uhamisho wa kimataifa kati ya mataifa ya Ulaya.
Aliweza kuchezea timu yake mara ya kwanza wakati wa msimu wa 2005-06 dhidi ya FC Crotone. Aliweza kuchezea Brescia mara 23 katika mashindano yote, akiingiza bao 3, kabla ya kusainiwa kwa West Ham.[2]
Mnamo Januari 26, 2009 Nsereko alitia saini na West Ham United kwa ada isiyojulikakna, iliyokadiriwa kuwa paundi milioni 9 kutegemea na mambo mengine,[3] juu mkataba wa miaka nne na nusu.[4] Alipewa shati namba 10 , kufuatia kuondoka kwa Craig Bellamy na kuendaManchester City, ambayo alichukua jina "Savio".[5] Mara yake ya kwanza kucheza mpira wa UIingereza f, Ligi Kuu na West Ham ilikuwa tarehe 28 januari 2009 nyumbani West Ham na kushinda 2-0 dhidi ya Hull City. [6] Alicheza sehemu muhimu katika ushindi wa West Ham dhidi ya Manchester City tarehe 1 Machi, 2009 kwa kusaidia Jack Collison kuingiza bao dakika 71 .[7]
Alishindwa kukaa katika West Ham, alicheza mechi ya kwanza vizuri lakini kushindwa kufunga bao yoyote mechi kumi alizoonekana. Aliuzwa Fiorentina kwa ada isiyojulikana, pamoja na Manuel da Costa kufuata njia hiyo nyingine kama sehemu ya mpango huo. West Ham abado ina haki ya asilimia 50 ya ada ya mchezaji huu.[8]
Katika ngazi ya kimataifa, Nsereko alishinda 2008 UEFA mpira wa Ulaya wa wachezaji walio umri chinin ya 19 l akichezea Ujerumani. Alijitokeza tena katika timu ya Ujerumani ya walio na umri chini ya 20 .[9]
Mamlaka ya Uganda ina tamaa ya Savio kuchezea timu ya taifa ya Uganda. Sheria mpya ambayo inaruhusu uraia wa nchi mbili unawezesha jambo hili.[10]
|isbn=
value (help).