Mlalo ni kata ya Wilaya ya Lushoto katika Mkoa wa Tanga, Tanzania. Msimbo wa posta ni 21721.
Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi walihesabiwa 7,589 [1]. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ina wakazi wapatao 8,143 waishio humo.
Kuna vijiji vya Mlalo, Msale, Kibandai, Ngazi, Mgwashi, Baghai na Bungoi.
Mlalo iko kwenye kimo cha mita 1450 juu ya usawa wa bahari magharibi mwa milima ya Usambara. Ni eneo lililokaliwa na Washambaa kabla ya enzi ya ukoloni[2].
Mnamo mwaka 1889 Wajerumani Baumann na Hans Meyer walikuta huko makao makuu ya mwene Sikinyassi[3] aliyetawala maeneo ya Usambara kaskazini.[4]
Kazi ya kanisa la Kilutheri kwenye milima ya Usambara ilianzia Mlalo. Mnamo mwaka 1891 wamisionari Walutheri Ernst Johanssen na Paul Wohlrab kutoka shirika la misioni Bethel katika Ujerumani walifika huko. Walikataa kusindikizwa na polisi ya kikoloni kwa sababu hawakutaka kuanzisha misioni yao kwa nguvu ya silaha[5]. Walipata kibali cha mwene Sikinyasi wakaanzisha kituo cha "Hohenfriedeberg"[6] (Kijerumani kwa mlima mrefu wa amani). Pamoja na kujenga kanisa, walianzisha pia kituo cha kuwahudumia wenye ukoma.
Kata za Wilaya ya Lushoto - Mkoa wa Tanga - Tanzania | ||
---|---|---|
Dule "M" | Gare | Hemtoye | Kilole | Kwai | Kwekanga | Kwemashai | Kwemshasha | Lukozi | Lunguza | Lushoto | Magamba | Makanya | Malibwi | Malindi | Manolo | Mbaramo | Mbaru | Mbwei | Migambo | Mlalo | Mlola | Mnazi | Mng'aro | Mtae | Mwangoi | Ngulwi | Ngwelo | Rangwi | Shagayu | Shume | Sunga | Ubiri |
Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Tanga bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Mlalo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno. |