Silaha za zama za mawe
Silaha ya karne ya 20

Silaha ni kifaa cha upiganaji dhidi ya wanadamu au wanyama.

Inafaa kumtisha, kumwumiza au kumwua adui au kumletea hasara nyingine inayokusudiwa.

Kusudi la silaha ni matumizi

Katika historia watu wameweka nguvu nyingi katika maendeleo ya silaha. Kila sayansi na kila teknolojia huangaliwa na watu kwa faida yake katika utengenezaji wa silaha.

Silaha zimepatikana tangu zama za mawe. Upanga, pinde na mshale pamoja na mikuki zilikuwa silaha kwa milenia nyingi lakini ziliboreshwa tena na tena.

Tangu nyakati za kati silaha za moto zilianza kuenea duniani na kuboreka. Bunduki, mzinga na bombomu zilibadilisha uso wa vita. Karne ya 20 iliongeza vifaru na ndege za vita pamoja na viumbe vya sayansi ya kisasa kama silaha za nyuklia.