Nchi inayoendelea ni neno linalotumika kuashiria taifa lenye kiwango cha chini cha nyenzo za uendelezi. Hakuna ufafanuzi hata mmoja wa neno hilo unaokubalika kimataifa, na viwango vya maendeleo vinaweza tofautiana kati ya nchi zinazosemekana kuwa zimeendelea, huku baadhi ya nchi zinazoendelea zikiwa na viwango vya juu vya maisha.[1][2]
Baadhi ya mashirika ya kimataifa kama Benki ya Dunia hutumia uainishaji wa kihesabu pekee. Benki ya Dunia huchukulia nchi zote zenye mapato ya chini na ya wastani kama "zinazostawi". Katika uainishaji wake wa hivi karibuni, uchumi wa nchi uligawanywa kwa kutumia Pato la Taifa kwa kila mwananchi. Mwaka wa 2008, Pato la Taifa kwa kila mwananchi chini ya US $ 11.905 zilihesabiwa kama zinazostawi[3]. Taasisi nyingine hutumia fasili zisizokuwa maalumu sana.
Nchi zenye uchumi ulioendelea zaidi kuliko nyingine zinazoendelea, lakini ambazo bado hazijaonyesha kikamilifu ishara za nchi iliyostawi huwekwa pamoja katika kundi la nchi zenye viwanda vingi. [4] [5][6] [7]
Kofi Annan, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, alifafanua nchi iliyostawi kama ifuatavyo. "Nchi iliyostawi ni nchi ambayo inaruhusu wananchi wake wote kufurahia maisha ya uhuru na afya katika mazingira salama." [8] Lakini kulingana na Divisheni ya Takwimu ya Umoja wa Mataifa,
Na inabainisha kuwa
Umoja wa Mataifa unabainisha pia
Kulingana na uainishaji wa IMF kabla ya Aprili 2004, nchi zote za Ulaya Mashariki (pamoja na nchi za Ulaya ya Kati ambazo zimo katika "Kikundi cha Ulaya Mashariki" katika taasisi za UN) pamoja na Umoja wa Kisovyeti (USSR) nchi za Asia ya Kati (Kazakhstan, Uzbekistan, Kyrgyzstan, Tajikistan na Turkmenistan) na Mongolia, hazikujumuishwa katika aidha maeneo yaliyostawi au yanayostawi, bali zilijulikana kama "nchi katika mpito"; hata hivyo kwa sasa huonekana (katika ripoti za kimataifa) kama "nchi zinazostawi".
Katika karne ya 21 kundi la awali la Four Asia Tigers [11] (Hong Kong, [11] [12] Singapore, [11] [12] Korea ya Kusini, [11] [12] [13] [14] na Taiwan [11] [12] ni kufikiriwa "yaliyoendelea" kanda au maeneo, pamoja na Kupro, [12] Israeli, [12] Malta, [12] na Slovenia, [12] ni kufikiriwa "nchi mpya zilizoendelea".
IMF hutumia mfumo wa uainishaji unaozingatia: "(1) per capita kiwango cha mapato, (2) mauzo ya mseto-hivyo mafuta nje kwamba wana high per capita GDP asingeweza kufanya advanced klassificering kwa sababu karibu 70% ya bidhaa zinazouzwa nje ni mafuta, na (3) shahada ya ushirikiano katika mfumo wa kifedha wa kimataifa. [15]
Benki ya Dunia huainisha nchi katika vikundi vinne vya mapato. Nchi za mapato ya chini zina Pato la Taifa kwa Kila mwananchi la US $ 975 au chini. Mapato ya chini katikati ni nchi zenye Pato la Taifa kwa Kila mwananchi la US $ 976 - $ 3,855. Nchi za Mapato ya Juu katikati ni nchi zenye Pato la Taifa kwa Kila mwananchi la US $ 3,856 - $ 11,905. Nchi za mapato ya Juu ni zile zenye pato zaidi ya $ 11,906. Benki ya Dunia huainisha nchi zote zenye mapato ya katikati na ya chini kama zinazostawi lakini inabainisha kuwa, "Matumizi wa neno hili ni kwa kurahisisha kazi tu; na hayakunuiwa kuashiria kuwa nchi zote katika kundi hilo zinapata maendeleo sawa au kwamba nchi zingine zimefikia kiwango kinachotakikana au mwisho wa hatua za maendeleo. Uainisho kwa mapato haumaanishi hicho ndicho kiwango haswa cha maendeleo kwa wakati huu[3].
Maendeleo ya nchi hupimwa kwa kutumia takwimu kama vile mapato kwa Kila mwananchi (GDP), urefu unaotarajiwa wa maisha, kiwango cha kujua kusoma na kadhalika. UN imeanzisha HDI, kiashiria cha jumla cha takwimu zilizotolewa hapo juu, ili kupima kiwango cha maendeleo ya katika nchi mahali takwimu zinapatikana.
Nchi zinazostawi kwa ujumla huwa ni nchi ambazo hazijapata mafanikio muhimu katikaa sekta ya viwanda ikilinganishwa na idadi ya raia wake, na ambazo, mara nyingi huwa na hali ya wastani au chini ya kiwango cha maisha. Kuna uhusiano mkubwa kati ya mapato ya chini na kiwango cha juu cha ukuaji wa idadi ya watu.
Maneno yanayotumika kujadili nchi zinazostawi hurejelea nia na miundo ya wanayoyatumia maneno haya. Maneno mengine yanayotumiwa wakati mwingine ni nchia ambazo hazijaendelea sana (LDCs), nchi ambazo zimeendelea kidogo zaidi (LEDCs), "mataifa yasiyoendelea" au mataifa ya Dunia ya Tatu na "mataifa ambayo hayajastawi kiviwanda". Kinyume na hayo, upande ule mwingine unaitwa nchi zilizostawi, nchi zilizoendelea zaidi kiuchumi (MEDCs), mataifa ya Dunia ya Kwanza na "mataifa yaliyostawi kiviwanda".
Ili kudhibiti neno la tasfida la zinazostawi, mashirika ya kimataifa yameanza kutumia neno Nchi ambayo haijastawi kiuchumi (LEDCs) kwa mataifa maskini ambayo hayawezi kuonekana kama yanayostawi. Yaani, LEDCs ndio kundi maskini zaidi kati ya LDCs. Hii inaweza kudhibiti dhidi ya imani kuwa kiwango cha maisha katika nchi zote zinazostawi ni sawa.
Dhana ya taifa linalostawi inapatikana, chini ya neno moja au lingine, katika mifumo ya kinadharia kadhaa yenye mitazamo tofauti - kwa mfano, nadharia za ukombozi kutoka ukoloni, teolojia ya ukombozi, Umarksi, kupinga ubeberu, na uchumi wa kisiasa.
Kuna ukosoaji kwa matumizi ya neno 'nchi inayostawi'. Jina hilo linadokeza kuwa chini kwa 'nchi inayostawi' ikilinganishwa na 'nchi iliyostawi', ambalo nchi nyingi kama hizo hazipendelei. Huchukulia kuna haja ya 'kustawi' kwa mtazamo wa 'Magharibi' wa maendeleo ya kiuchumi ambayo nchi nyingi, kama vile Cuba, zimechagua kutofuata. Hivyo basi Cuba inabakia kuainishwa kama nchi 'inayoendelea' kutokana na Pato lake dogo la Taifa lakini ina kiwango cha chini cha vifo vya watoto wachanga na kiwango cha juu cha elimu kuliko Marekani[16].
Neno 'zinazostawi' linadokeza kuwa na mwendo na haibainishi kwamba maendeleo yanaweza kuwa yanashuka au kusimama katika baadhi ya nchi, hasa zile za kusini mwa Afrika yaliyoathirika zaidi na VVU / UKIMWI.
Jina hili linadokeza usawa kati ya nchi hizo ambazo zinatofautiana sana. Pia linadokeza usawa katika nchi hizo ilhali utajiri na afya vya vikundi vilivyo tajiri na maskini vinatofautiana sana.
Nchi zifuatazo zinachukuliwa kama zinazoibukia na kustawi kiuchumi kulingana na ripoti ya mtazamo wa uchumi wa dunia ya Shirika la Fedha la Kimataifa ya Oktoba 2009[17].
Nchi mara nyingi huwekwa ndani ya makundi manne hafifu ya maendeleo. Kila kikundi kinajumuisha nchi zilizotajwa katika makala yake. Neno "taifa linalostawi", sio lebo ya aina maalumu au sawa ya tatizo.
((cite book))
: Unknown parameter |coauthors=
ignored (|author=
suggested) (help); Unknown parameter |dead-url=
ignored (|url-status=
suggested) (help)CS1 maint: location (link)
((cite web))
: Check date values in: |date=
(help)
((cite book))
: Check date values in: |year=
(help)
((cite book))
: Check date values in: |year=
(help)
((cite web))
: Check date values in: |date=
(help)
South-South cooperation and Third Worldism | |
---|---|
The Third World | Emerging markets · Emerging Markets Index · Newly industrialized country · Landlocked developing countries · ACP countries · Least Developed Countries · Heavily Indebted Poor Countries · Fourth World |
Organizations | G-77 ·G-15 ·G-20 · G-24 · G-33 · G-11 · G90 ·Umoja wa Nchi za Asia ya Kusini-Mashariki ·SAARC · Umoja wa Afrika ·Melanesian Spearhead Group ·United Nations Industrial Development Organization ·UNDP ·United Nations Conference on Trade and Development ·Arab Monetary Fund · Asian Clearing Union · Asian Development Bank · Bank of the South · South Centre ·Third World Network |
Geopolitics | Decolonization · Ukoloni Mamboleo · Third World debt · Vita baridi · IBSA ·BASIC ·BRIC · Next Eleven · Global digital divide · Flying Geese Paradigm · World Conference against Racism · Durban Review Conference ·Fair trade |