Peru
Ramani ya Peru
Peru
Machu Picchu

Peru (pia Peruu) ni nchi ya Amerika Kusini upande wa magharibi ya bara.

Imepakana na Ekuador, Kolombia, Brazil, Bolivia na Chile. Kuna mwambao wa Pasifiki.

Historia

Peru ilikuwa koloni la Hispania kati ya miaka 1532 na 1821.

Kabla ya kuja kwa Wahispania, Peru ilikuwa kitovu cha Dola la Inka.

Watu

Hadi leo kuna idadi kubwa ya Waindio (45%) wanaotunza utamaduni wao, mbali ya machotara Waindio-Wazungu (37%). Utafiti wa DNA yao unaonyesha urithi wa Kiindio umechangia 79.1% za DNA ya wakazi wa leo. Wazungu wenyewe ni 15% tu.

Lugha rasmi ni Kihispania (84.1%), Kiquechua (13%) na Kiaymara (1.7%).

Upande wa dini, Wakatoliki ni 81.3% na Waprotestanti 12.5%.

Tazama pia

Marejeo

Viungo vya nje

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Peru
Nchi na maeneo ya Amerika Kusini

Argentina | Bolivia | Brazil | Chile | Ekuador | Guyana | Guyani ya Kifaransa | Kolombia | Paraguay | Peru | Surinam | Uruguay | Venezuela

Makala hii kuhusu maeneo ya Amerika Kusini bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Peru kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.