"Bernadeta" (Marie-Bernarde) Soubirous (Lourdes, Hautes-Pyrénées, 7 Januari 1844 - Nevers, Nièvre, 16 Aprili 1879) alikuwa mtawa wa Kanisa Katoliki nchini Ufaransa.
Tarehe 14 Juni 1925 Papa Pius XI alimtangaza mwenye heri[1] na tarehe 8 Desemba 1933 mwenyewe alimtangaza mtakatifu bikira.[2]
Sikukuu yake imepangwa tarehe ya kifo chake[3] au 18 Februari, siku ambapo Bikira Maria alimuahidia kumpatia heri, ingawa si katika maisha ya duniani.
Mtoto wa familia fukara sana, anajulikana hasa kwa njozi za Bikira Maria alizojaliwa kwenye pango la Massabielle kati ya tarehe 11 Februari na 16 Julai 1858, akiwa na umri wa miaka 14. Hatimaye Maria alijitambulisha kama Kukingiwa Dhambi ya Asili, sifa yake iliyotangazwa na Papa Pius IX kuwa dogma ya imani Katoliki miaka 4 ya nyuma.[4]
Ingawa viongozi wa Kanisa walikuwa na shaka kwanza, utafiti uliwafanya wakubali ukweli wa tukio hata inaanzishwa adhimisho la Bikira Maria wa Lourdes na patakatifu palipojengwa mahali pake pamekuwa mahali pa hija panapofikiwa na watu zaidi ya milioni 5 kwa mwaka.[5]
Baada ya kujiunga na utawa na kustahimili kwa unyenyekevu matatizo mengi upande wa mwili (kipindupindu, pumu kali, kifua kikuu n.k.) na wa nafsi (dhuluma kutoka kwa watu wasioamini njozi zake au waliomuonea kijicho kwa hizo), alifariki akiwa na umri wa miaka 35 tu.
On may 13, 1913, Pope Pius X signed the decree introducing the cause of Bernadette's beatification. She was beatified on June 14th, 1925. Eight years later, it was on the feast of the Immaculate Conception, December 8, 1933 she was canonized by Pope Pius XI.Check date values in:
|date=, |accessdate=
(help)
|date=
(help)
|date=
(help)
|accessdate=
(help)
|accessdate=
(help)
|date=
(help)
|date=
(help)
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |