Uwanja wa michezo (Kilat. + Kiing. stadium) ni mahali pa mashindano ya michezo. Mara nyingi umezungukwa na majengo ambayo yanaweza kufunguliwa juu na kuwezesha umma kutazama onyesho hilo kwa kutumia nafasi za kusimama au kukaa. Viwanja mara nyingi hutumiwa pia kwa matamasha na mikutano ya hadhara.
Viwanja vya michezo vilipatikana tayari katika miji mingi ya Ugiriki ya Kale ambako mashindano yalitekelezwa kwa heshima ya miungu. Mashuhuri hasa vilikuwa viwanja vya Olimpia na Delfi[1].
Katika Roma ya Kale viwanja vilitumiwa hasa kwa matamasha ya mapigano na uwindaji. Mfano mashuhuri ni Koloseo wa Roma. Jengo hili lilikuwa kielelezo wa viwanja vingi vya kisasa.
Makala hii kuhusu mambo ya michezo bado ni mbegu. Je, unajua kitu zaidi kuhusu Uwanja wa michezo kama historia yake, uenezi au kanuni zake? Labda unaona katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine habari zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |