Unyanyasaji wa kingono ni aina ya unyanyasaji unaohusisha matumizi ya matamshi ya ngono ya wazi au ya siri, ikiwa ni pamoja na ahadi zisizohitajika na zisizofaa za zawadi kwa kubadilishana na faida za ngono.[1]
Unyanyasaji wa kijinsia unajumuisha vitendo mbalimbali kama vile maneno yasiyofaa kwa jinsia nyingine. Unyanyasaji unaweza kutokea katika mazingira mbalimbali ya kijamii kama vile sehemu za kazi, nyumbani, shuleni, au kwenye taasisi za kidini.
Waathirika wanaweza kuwa wa jinsia yoyote[2], ingawa mara nyingi zaidi ni wanawake.
Makala hii kuhusu mambo ya sheria bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Unyanyasaji wa kijinsia kama historia yake au uhusiano wake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |