Ukame (kwa Kiingereza "Drought") ni hali ya hewa ya sehemu au mahali fulani inayofanya pakose maji ya kutosha kwa muda mrefu[1]. Kwa kawaida hii inamaanisha kipindi ambako kuna mvua kidogo, au kupungukiwa kwa usimbishaji mwingine kama theluji.
Ukame unatokea pia pale ambako watu na kilimo wanategemea maji kwa umwagiliaji na vyanzo vingine vya maji vinakauka.
Ukame unaweza kuhatarisha uhai wa mimea, wanyama na watu, ambao wote wanahitaji maji.
Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.
|