Papa Callixtus I alikuwa Papa kuanzia takriban 218 hadi kifodini chake takriban 222[1].
Alimfuata Papa Zefirino akafuatwa na Papa Urbano I.
Aliwahi kuwa mtumwa[2], lakini mwaka 199 Papa Zefirino alimfanya shemasi na mshauri wake mkuu.
Kisha kuchaguliwa kuwa Papa, kwa upole wake alifaulu kuvuta wafuasi wa uzushi na mafarakano mbalimbali, akifundisha kwamba Kanisa lina mamlaka ya kusamehe dhambi zote. [3][4] Kutokana na msimamo huo, inasemekana waliokuwa wakali zaidi walimchagua Hipoliti wa Roma kama antipapa wa kwanza.[5]
Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu mfiadini.
Sikukuu yake ni tarehe 14 Oktoba[6].
Makala hii kuhusu Papa fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Papa Callixtus I kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |