Kufuata Fasheni (1794), katuni ya James Gillray.
Mwanamitindo nchini Tanzania

Mitindo (au fasheni kutoka Kiingereza fashion) ni njia ya mtu, kundi au jamii kufanya au kuwasilisha jambo kwa namna maalumu. Kwa mfano kufanya jambo harakaharaka, polepole, kwa taratibu fulanifulani na kadhalika. Halafu hiyo namna maalumu inaenea katika jamii, hasa upande wa mavazi. Mitindo inabadilikabadilika kadiri ya mahali na nyakati.[1][2][3]

Kuna watu maalumu ambao wanabuni mitindo mipya, wanaionyesha na kuisambaza, mara nyingi kwa faida kubwa kiuchumi.

Kutokana na utandawazi, siku hizi mitindo inaenea duniani kote, hasa kutoka nchi tajiri kwenda nchi maskini, na pengine inaharibu maadili na utamaduni.

Tanbihi

  1. Fashion (2012, March 29). Wwd. (n.d.). Retrieved from http://www.wwd.com/fashion-news.
  2. Undressing Cinema: Clothing and identity in the movies – Page 196, Stella Bruzzi – 2012
  3. For a discussion of the use of the terms "fashion", "dress", "clothing", and "costume" by professionals in various disciplines, see Valerie Cumming, Understanding Fashion History, "Introduction", Costume & Fashion Press, 2004, ISBN 0-89676-253-X

Marejeo

Viungo vya nje

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Mitindo
Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mitindo kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.