Metali za udongo alikalini ni mfulizo wa kikemia katika mfumo radidia unaounganisha elementi za kundi la pili yaani elementi thabiti Berili (Be), Magnesi (Mg), Kalisi (Ca), Stronti (Sr) na Bari (Ba) pamoja na elementi nunurifu ya radi (Ra) ambayo ni tokeo la mbunguo wa elementi nyingine.

Jina

[hariri | hariri chanzo]

Jina la "metali za udongo alikalini" linatokana na historia ya uchumbuzi wa elementi hizo. Zilianza kutambuliwa katika umbo la oksidi zake. Kampaundi hizo ziliitwa "udongo" au "ardhi" na wanakemia wa kale kama dutu zisizokuwa metali wala kuathiriwa na joto na zisiyomumunyika katika maji. Zikikorogwa katika maji zinaonyesha tabia ya alikalini.

Mfaransa Antoine Lavoisier alitambua mwaka 1789 ya kwamba ardhi hizo hazikuwa "elementi" bali kampaundi. Aliamini ya kwamba msingi wake zilikuwa elementi alizozitaja kama "elementi za udongo" zinazojenga chumvi mbalimbali akahisi ya kwamba labda udongo hizo ni oksidi za metali. Hii ilithibitishwa mwaka 1808 na Mwingereza Humphry Davy kwa njia ya elektrolisisi.

Tabia

[hariri | hariri chanzo]

Metali za udongo alikalini ni metali laini zenye rangi nyeupe-fedha. Zinamenyuka na halojini kuwa aina za chumvi; mmenyuko na maji husababisha kutokea kwa hidroksidi alikalini.

Hazimenyuki haraka na vikali kama metali alikalini.

Zote zina elektroni mbili katika mzingo elektroni wa nje. Kwa hiyo zinaelekea kuachana na elektroni hizo kuingia katika hali kuwa ioni yenye chaji ya chanya.

Mmenyuko

[hariri | hariri chanzo]

Mmenyuko huongezeka kadiri ya namba atomia au ukubwa wa atomi:

Kutokea

[hariri | hariri chanzo]

Elementi hizo kwa jumla ni asilimia 4.16 za masi ya ganda la dunia. Kati ya metali za udongo alikalini ni: