Mchapuko (pia mchapuo, kwa Kiingereza acceleration) ni istilahi ya fizikia inayotaja badiliko la kasi au zaidi kasimwelekeo ya kitu kwa kipindi fulani. Mchapuko unafafanuliwa kuwa badiliko la kasimwelekeo (velositi) linalogawiwa kwa badiliko la wakati.

Mchapuko unatokea kama gimba linaongeza kasi, linapunguza kasi au linabadilisha mwelekeo wake. Mfano gari linalopiga mbio, linalopigwa breki au kupiga kona linaona mchapuko.

Kipimo cha SI cha mchapuko ni m/s2 yaani mraba wa mita kwa sekunde.

Makala hii kuhusu mambo ya fizikia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mchapuko kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.