Kleri ni kundi la watu wanaoongoza dini fulani. Jina linatokana na neno la Kigiriki "κλῆρος" - klēros, "bahati", "sudi" au also "urithi".
Katika madhehebu mengi ya Ukristo kleri ina daraja takatifu tatu: kuanzia juu ni uaskofu, upadri na ushemasi. Hata hivyo baadhi yao wanapewa pia majina mengine kulingana na huduma zao, kwa mfano: Papa, kardinali, monsinyori, abati, kanoni, arkimandrita n.k.
Katika Uislamu hakuna ukuhani, hivyo uongozi unategemea tu elimu ya dini: kuna mufti, imamu, ustadhi n.k.
Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |