Kichocho (bilharzia, schistosomiasis) | |
---|---|
Mwainisho na taarifa za nje | |
Specialty | Infectious diseases |
ICD-10 | B65. |
ICD-9 | 120 |
MedlinePlus | 001321 |
MeSH | D012552 |
Kichocho, kisalisali au kisonono cha damu (pia schistosomiasis au bilharzia) ni ugonjwa ambao minyoo midogo ya aina ya Schistosoma (minyoo-kichocho) inaingia mwilini na kusababisha mwasho wa ngozi katika viungo mbalimbali, homa, udhaifu na baada ya muda damu katika kinyesi au mkojo na maumivu tumboni. [1]
Minyoo-kichocho inaendelea kwa hatua zifuatazo:
Kwa hiyo maisha ya Schistosoma na nafasi ya maambukizi huhitaji:
Kwa hiyo njia ya kuambukizwa ni kuingia katika maji yenye konokono walioambukizwa. Siku hizi karibu kila ziwa au bwawa katika Afrika huwa na hatari ya kichocho; hatari inapungua katika mito yenye mwendo wa maji au katika sehemu ya maziwa makubwa ambako kuna pwani pana ya mchanga bila mimea iliyo chakula cha konokono.
Taratibu wa kukinga dhidi ya maradhi haya ni pamoja na upatakanaji wa maji safi na upungufu wa idadi ya konokono. Katika maeneo ambako maradhi yanaambukiza zaidi, makundi ya watu wengi wanaweza kutibiwa kwa wakati mmoja, kwa kuwapa mara moja kwa mwaka dawa iitwao praziquantel. Utaratibu huo unakusudia kupunguza idadi ya watu wanaoambukizwa na kwa hivyo kupunguza kuenezwa kwake maradhi yenyewe.
Praziquantel ni dawa inayopendekezwa na Shirika la Afya Duniani kwa ajili ya wale wanaojulikana kuambukizwa.[5].
Ugonjwa na kidusia chake vilitambuliwa mara ya kwanza mwaka 1851 na tabibu Mjerumani Theodor Bilharz alipochunguza maiti katika hospitali moja mjini Kairo, nchini Misri . Kwa hiyo ugonjwa umejulikana pia kwa jina la Bilharzia.
Makala hii kuhusu mambo ya tiba bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Kichocho kama sababu yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |