Justiniani I anavyoonekana katika mozaiki ya wakati wake katika Basilika la San Vitale, Ravenna, Italia.

Justiniani I au Justiniani Mkuu (jina kamili kwa Kilatini: Flavius Petrus Sabbatius Iustinianus Augustus; kwa Kigiriki Φλάβιος Πέτρος Σαββάτιος Ἰουστινιανός, Flávios Pétros Sabbátios Ioustinianós; Tauresium, Dardania,[1] leo nchini Masedonia Kaskazini[2] takriban 482 - Konstantinopoli, leo nchini Uturuki, 14 Novemba, 565) alikuwa kaisari wa Dola la Bizanti kuanzia mwaka wa 527 hadi kifo chake.

Justiniani alijitahidi kurudisha Dola la Roma katika fahari yake ya zamani (renovatio imperii, yaani kufanya upya dola) na kwa ajili hiyo alipigania upande wa magharibi dhidi ya wavamizi. Hata hivyo alifaulu kiasi tu.[3]

Mke wake na malkia wa Bizanti aliitwa Theodora; aliaga dunia mwaka wa 548. Hawakuwa na watoto walioishi. Hivyo Justiniani I alifuatwa kama kaisari na mpwa wake Justin II.

Huheshimiwa na Wakristo Waorthodoksi na Walutheri kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 14 Novemba au 27 Novemba[4].

Tazama pia

Tanbihi

  1. Britannica Concise Encyclopedia, Encyclopædia Britannica, Inc., 2008, ISBN|1593394926, p. 1007.
  2. History of the Later Roman Empire from Arcadius to Irene, Volume 2, J. B. Bury, Cosimo, Inc., 2008, ISBN|1605204056, p. 7.
  3. J. F. Haldon, Byzantium in the seventh century (Cambridge, 2003), 17–19.
  4. In various Eastern Orthodox Churches, including the Orthodox Church in America, Justinian and his empress Theodora are commemorated on the anniversary of his death, 14 November. Some denominations translate the Julian calendar date to 27 November on the Gregorian calendar. The Calendar of Saints of the Lutheran Church–Missouri Synod and the Lutheran Church–Canada also remember Justinian on November 14.

Vyanzo

Marejeo mengine

Viungo vya nje

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Justiniani I
Search Wikisource Wikisource has original text related to this article:
Makala hii kuhusu Kaizari fulani wa Bizanti bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Justiniani I kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.