Hali ya ushirika kamili inamaanisha kuwa ibada zote zinazofanywa katika kanisa moja zinatambuliwa na mengine. Baadhi ya makanisa hayo yanatumia jina "Anglikana", yakitambua uhusiano wa pekee na Kanisa la Uingereza; neno la KilatiniAnglicana linamaanisha "la Uingereza". Katika maeneo mengine Waanglikana wanatumia jina la "Kanisa la Kiaskofu" (Episkopali, Kiingereza: episcopalian).
Askofu Mkuu wa Canterbury aliye mkuu wa kidini wa Kanisa la Uingereza anatambuliwa kama ishara ya umoja huo. Hata hivyo hana mamlaka rasmi nje ya Uingereza yenyewe.
Ramani ya Dunia inayoonyesha majimbo ya Jumuiya Anglikana:
Majimbo ya kitaifa Kanisa la Kiaskofu la Marekani (Episcopal Church) Kanisa la Jimbo la West Indies Kanisa Anglikana katika Amerika ya Kati Kanisa Anglikana ya Amerika ya Kusini Kanisa Anglikana ya Afrika ya Kusini Kanisa la Jimbo la Afrika ya Kati Kanisa la Jimbo la Afrika ya Magharibi
Kanisa la Kiaskofu huko Yerusalemu na Mashariki ya Kati Kanisa la Jimbo la Bahari ya Hindi Lanisa Anglikana huko Aotearoa, New Zealand na Polynesia Kanisa la Jimbo la Melanesia Dayosisi ya Ulaya ya Kanisa la Uingereza Makanisa nje ya jimbo chini ya Askofu Mkuu wa Canterbury Kanisa la Jimbo la Asia Kusini Mashariki Maeneo yasiyo na makanisa ya Kianglikana
Zingatia kwamba Kanisa la Eire linahudumia Eire ya Kaskazini (Northern Ireland) pamoja na Jamhuri ya Eire; Kanisa Anglikana la Korea linahudumia Korea Kusini na kinadharia (si hali halisi) pia Korea Kaskazini. Waanglikana wa Uhindi wamegawiwa kwa majimbo ya Kanisa la Uhindi Kaskazini na Kanisa la Uhindi Kusini. Dayosisi katika Ulaya (zamani Dayosisi ya Gibraltar katika Ulaya) ni sehemu ya jimbo la Canterbury likiwa pia na parokia katika Ureno na Hispania. Kanisa la Kiaskofu la Marekani lina parokia pia katika Ulaya.
Jumuiya hiyo inafanywa na majimbo yanayojitawala; kila jimbo lina dayosisi ndani yake zinazosimamiwa na askofu wake. Kuna pia maeneo kadhaa yasiyo na hadhi ya jimbo.