Fasihi (kutoka neno la Kiarabu فصاحة, fasaha kwa maana ya ulimbi au "literacy" kwa Kiingereza) ni utanzu (tawi) wa sanaa ambao hutumia lugha ya mazungumzo au maandishi ili kufikisha (kuwasilisha) ujumbe kwa hadhira husika. Ni ufundi wa kuwasilisha mawazo au ujumbe ulio katika fikra za binadamu.Fasihi ni sanaa inayotumia lugha kwa ubunifu kuwasilisha masuala kuhusu maisha ya binadamu na mazingira

Vipengele vinavyounda fani ya fasihi ni kama ifuatavyo: fani ni umbo la nje la kazi ya fasihi; maudhui ni umbo lake la ndani.

Fani

Katika kazi yoyote ya fasihi ni lazima pawepo na ustadi wenye kuleta mvuto fulani kwa hadhira (wasikilizaji au wasomaji) husika. Ustadi (ufundi) huo unaovutia hadhira huitwa fani, ambayo hujumuisha mambo kama vile:

Maudhui

Pamoja na fani, kazi yoyote ya fasihi huwa na ujumbe na malengo mbalimbali ambayo hukusudiwa yaifikie jamii husika. Yale yote ambayo msanii wa kazi ya fasihi anakusudia yaifikie jamii husika huitwa maudhui. Maudhui ya kazi ya fasihi hujumuisha:

Sifa za fasihi

Dhima za fasihi katika jamii

Fasihi hufanya kazi mbalimbali katika maisha:

Aina za fasihi

Fasihi ndiyo aina pekee ya sanaa inayotumia lugha kujitambulisha au kujitofautisha na aina nyingine za sanaa. Kuna aina kuu mbili za fasihi nazo ni:

Fasihi hizi zina dhima sawa katika jamii ingawa ni tofauti. Utofauti kati ya fasihi simulizi na fasihi andishi hujitokeza katika uwasilishwa wake katika jamii husika.

Fasihi simulizi

Fasihi simulizi ni aina ya fasihi ambayo hutumia mazungumzo ya mdomo ili kufikisha ujumbe kwa hadhira. Aina hii ya fasihi ndiyo iliyokuwapo tangu zamani kabisa mwanadamu alipoanza kuishi yaani ilianza pale mwanadamu alipochangamana na wenzake katika kufanya mambo mbalimbali mfano,shughuli za biashara,kilimo,na nyinginezo.

kuna tanzu nne za fasihi simulizi .ie;

Sifa za fasihi simulizi

Dhima za fasihi simulizi

Kufanana kwa fasihi simulizi na fasihi andishi

Kimsingi fasihi ni moja ingawa imegawanyika katika sehemu kuu mbili, yaani, fasihi simulizi na fasihi andishi. Mbali na mgawanyiko huo kuna mambo ambayo yanafanana katika fasihi zote mbili. Mambo hayo ni pamoja na:

Tofauti kati ya fasihi simulizi na fasihi andishi

Na. Kipengele Fasihi simulizi Fasihi andishi
1 Uwasilishwaji Fasihi simulizi huwasilishwa kwa njia ya masimulizi ya mdomo pamoja na vitendo Fasihi andishi huwasilishwa kwa njia ya maandishi bila vitendo
2 Umri Fasihi simulizi ni kongwe kuliko fasihi andishi Fasihi andishi ni changa kuliko fasihi simulizi
3 Umilikaji Fasihi simulizi humilikiwa na jamii nzima, ni mali ya jamii Fasihi andishi humilikiwa na mwandishi, ni mali ya mwandishi
4 Tanzu Fasihi simulizi ina tanzu nyingi kuliko fasihi andishi Fasihi andishi ina tanzu chache kuliko fasihi simulizi
5 Hadhira hadhira ina uhusiano wa moja kwa moja na fanani yaani kuna hadhira hai hadhira inayoshirika haina uhusiano wa moja kwa moja na fanani
6 Mabadiliko Fasihi simulizi hubadilika haraka kutegemeana na mahitaji ya hadhira na wakati Fasihi andishi haibadiliki haraka kutegemeana na mahitaji ya hadhira na wakati
7 Utunzi Fasihi simulizi hutungwa kwa muda mfupi Fasihi andishi hutungwa kwa muda mrefu
8 Mazingira ya uwasilishaji wake (mandhari) Huambatana na tukio maalumu la jamii Kusoma au kusomewa ni ya kufikirika au mahali popote
9 Marekebisho Mtunzi/msimulizi anaweza kurekebisha kazi yake wakati wa kuwasilisha au baadaye kidogo Kitabu kikishaandikwa ni vigumu kukifanyia marekebisho mpaka toleo jipya litakapoandikwa
10 Uhifadhi Huhidhiwa kwa njia ya kichwa (kichwani) kwa sehemu kubwa na sehemu ndogo sana huhifadhiwa kwenye maandishi, vinasa sauti au kanda mbalimbali za kurekodi Huhifadhiwa kwa njia ya maandishi (vitabu)
11 Gharama Fasihi simulizi ina gharama ndogo ukilinganisha na fasihi andishi Fasihi andishi ina gharama kubwa ukilinganisha na fasihi simulizi
12 Wahusika Fasihi simulizi mara nyingi hutumia wahusika wa kubuni wasio binadamu Fasihi andishi hutumia wahusika wa kubuni ambao mara nyingi ni binadamu
13 Uhai Fasihi simulizi ni hai kuliko fasihi andishi Fasihi andishi si hai kuliko fasihi simulizi

Viungo vya nje

Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Fasihi kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.