Bao (au Bao la Kiswahili au Bao la Zanzibar) ni mchezo wa jadi wa aina ya mankala unaochezwa na wachezaji wawili.
Mchezo wa Bao umesambaa sana katika nchi za Afrika Mashariki, hasa Tanzania Bara (Tanganyika), Zanzibar na Kenya, lakini pia Rwanda, Komori, Malawi[1] pamoja na baadhi ya maeneo ya DR Congo na Burundi.
Nchini Tanzania, hasa Zanzibar, wachezaji wanashindana mara kwa mara na washindi wanaitwa mabingwa, lakini pia mafundi, wasanii na wanaheshimiwa sana.
Jina lenyewe "Bao" ni neno la Kiswahili kwa "ubao" au "mchezo wa ubao".
Bao ni mchezo mgumu kuliko michezo yote ya aina ya mankala. Inajulikana sana kuwa mancala mashuhuri katika suala la utata na kina kimkakati, [2] na imeibua shauku kwa wasomi wa taaluma kadhaa, ikijumuisha nadharia ya mchezo, nadharia changamano, na saikolojia.[3]
Nje ya Afrika watalaamu wa michezo na wanasaikolojia wanavutiwa sana na mchezo huu.
Mashindano rasmi yanafanyika Tanzania, Zanzibar, Lamu (Kenya), na Malawi, na Tanzania Bara na Zanzibar zote zina vyama vyao vya Bao, kama vile Chama cha Bao kilichoanzishwa mwaka wa 1966.
Aina nyingine za Bao ni Sono ya Wagogo, Engesho ya Wamasai, n.k.
Mchezo wa Bao huchezwa na mchezaji wawili; mmoja kila upande. Mchezaji mmoja anaitwa Kaskazini (K) na mwingine Kusini (S).
Bao linachezwa kwa kutumia kipande cha mbao kiliochimbwa mashimo 32 yaliyopangwa kwa mistari minne.
Mashimo mawili ya upande wa juu yanamilikiwa na mchezaji anayeitwa
Kaskazini, mashimo mawili ya chini yanamilikiwa na mchezaji anayeitwa
Kusini.
Mistari miwili ya mashimo ya katikati inaitwa mistari ya mbele (au ya
ndani) mistari miwili ya mashimo ya nje inaitwa mistari ya nyuma (au
ya nje).
Shimo la tano kutoka upande wa kushoto kwenda kulia kwa mchezaji la
kila mstari wa ndani linaitwa nyumba na, kwenye bao kadhaa,
lina umbo tofauti.
Kwenye bao kadhaa kuna mashimo mawili ya ziada ya kuhifadhia kete
(au namu, au kombwe au vijiwe) za wachezaji. Tunayaita ghala
Mashimo haya yapo upande wa kulia wa kila mchezaji
au mbele ya kila mchezaji.
Bao huchorwa jinsi vifuatavyo:
0 | |||||||
0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
-------------------------------- | |||||||
0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
0 |
ambapo mashimo yanaonyeshwa kwa kuandika namba ya idadi ya kete yanazo
ndani yake (0 inaonyesha shimo lisilo na kete yoyote) na ghala zipo
upande wa kulia wa kila mchezaji.
Mashimo wa upekee.
Katika bao zipo aina 5 za mashimo yenye kazi tofauti.
X | |||||||
0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
& | % | 0 | # | 0 | 0 | % | & |
-------------------------------- | |||||||
& | % | 0 | 0 | # | 0 | % | & |
0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 | 0 |
X |
Majina yao,
X, ghala
(yenye kete za kutia katika bao, yaani 'kete za mikononi' au 'namu').
#, nyumba.
&, kichwa.
%, kimbi.
0, mashimo ya kawaida.
Kuanzia sasa alama zilizotangulia (X, #, &, %) hazitatumika tena
kwenye michoro ya Bao. Badala yao itatumika namba ya idadi ya kete yanazo
ndani ya kila mshimo (0 inaonyesha shimo lisilo na kete yoyote).
Kete (au namu au komwe au vijiwe au mbegu) za kuchezea ni 64.
Mshindi ni yule mchezaji wa kwanza anayekula kete zote
zilizomo mashimoni mwa mstari wa ndani wa mshindani wake au ambaye
anafanya mshindani wake asiweze kucheza.
Msingi wa Bao ni kusambaza kete. Maana ya kusambaza ni kuhamisha kete moja
moja kutoka shimo fulani ndani mashimo yanayofuata kwenye mistari yake
kuelekea kutoka upande wa kushoto kuenda kulia (mwendo wa saa) au kutoka
upande wa kulia kuenda kushoto (kinyume na mwendo wa saa).
Mchezaji anaruhusiwa kula ambapo baada ya kusambaza kete zake shimo la mwisho:
Mchezaji anakula kwa kuchukua kete zote za mshindani wake zilizomo
ndani ya shimo linalotazamana na shimo lake la mwisho na anazihamisha
ndani ya mashimo yake ya mstari wa kwanza.
Duru ya mchezaji mmoja ni mfululizo wa uhamishaji wa kete na ulaji.
Duru inakwisha wakati mchezaji anatia kete yake ya mwisho ndani ya shimo lisilo na kete au (tutaeleza baadaye tukio hili) ndani ya nyumba au ndani ya shimo linalotakatia.
Mwishoni wa duru moja zamu ya kucheza ni ya mpinzani.
Ambapo shimo la mwisho la usambazaji lina kete (k.m. baada ya usambazaji shimo lina kete mbili au zaidi) na hairuhusiwi kula, mchezaji anachukua kete zake zilizomo ndani ya shimo hili la mwisho akaendelea kusambaza kuanzia shimo linalofuata kwa kushika mwelekeo wake. Kitendo hicho kinaitwa kuendelea au kusafiri.
Kama mchezaji hawezi kula inambidi atakate.
Mchezaji asiyeanza duru kwa kitendo cha kula, haruhusiwi kula wakati
wa duru nzima, yaani mpaka mwisho wa zamu yake.
Wakati wa kutakata, mchezaji anaendelea
mpaka mwisho wa kitendo cha kutakata.
Wakati wa kutakata, mwelekeo wa duru huwezi kubadiliki.
Kanuni zaidi zinategemea na hatua ya mcheso: kunamua au mtaji.
Mchezaji anayeanza duru kwa kitendo cha kula, hata baadaye anaruhusiwa kula tena wakati wa kitendo cha kuendelea, kwa kufuata kanuni za kitendo cha kula
Wakati unaoendelea toka mwanzo wa mchezo mpaka kete zote kuwa mashimoni na kumalizika mkononi unaitwa hatua ya kunamua.
Mwanzoni kila mchezaji ana 22 kete ndani ya mashimo ya kuhifadhia kete
(ghala), kete 6 ndani ya nyumba na kete 2 ndani ya mashimo
yanayofuata nyumba kuelekea upande wa mkono wa kulia wa mchezaji.
Anayeanza kucheza anaitwa Kusini (S).
Wakati wa hatua hii, mchezaji anachukua kete moja kutoka shimo la
kuhifadhia kete na anaiweka ndani ya shimo moja la mstari wa ndani.
Mchezaji anaruhusiwa kuweka kete ndani ya nyumba yake ijapo
inawekezana kula kete za mpinzani zilizomo ndani ya shimo linatazamana
na nyumba.
Mfano:
Mchezaji wa Kusini inambidi achukue kete moja kutoka ghala yake yenye kete 18 ('kete za mikononi') na anaweza kuiweka ndani ya shimo linalo kete 2 au ndani ya shimo linalo kete 1.
Kama mchezaji anaweza kula ni lazima aweke kete aliyochukua kutoka ghala yake ndani ya shimo linawezesha kula kwa kufuata kanuni ya Kitendo cha kula.
Mfano:
Mchezaji wa Kusini inambidi achukue kete moja kutoka ghala
yake yenye kete 14 (yaani 'kete moja ya mkononi') na aiweke ndani
ya shimo lenye kete 2 au ndani ya shimo moja lenye kete 3 au ndani ya
nyumba yake (mchaguo mzuri zaidi kwa sababu mchezaji wa
Kaskazini angeweza kula nyumba hii!).
Mchezaji wa Kusini lazima achukue kete moja kutoka ghala yake (au kete
moja ya mkononi) na aiweke ndani ya shimo linalo kete 3, hivi anakula kete
3 za mpinzani wake.
Anaweza kusambaza kete alizokula kuanzia kichwa cha kushoto:
Mfano:
au kuanzia kichwa cha kulia:
Wakati wa hatua ya kunamua, hairuhusiwi kutakata (kitendo kinachoruhusiwa kama haiwezekani kula) toka shimo la mstari wa nje (au nyuma).
Mchezaji wa Kusini anaruhusiwa kucheza shimo linalo kete 4,
haruhusiwi kucheza kuanzia nyumba.
Kama mashimo yote ya mstari wa nje hayana kete ndani yao,
isipokuwa nyumba tu, basi mchezaji anaweka kete aliyochukua kutoka
shimo la kuhifadhia ndani ya nyumba na anachukua kete mbili kutoka
nyumba akazihamisha ndani ya mashimo yanayofuata nyumba kuelekea
kulia au kushoto.
Mfano:
Mchezaji wa Kusini anaweza kucheza hivi:
au hivi:
Mchezaji wa Kusini haruhusiwi kutakata kuanzia shimo
lenye kete moja tu.
Wakati wa mwanzo wa mchezo wachezaji wote wawili wanamiliki nyumba zao.
Hatua ya mtaji inaanza kama kete zote 64 zimo mashimoni na kete za mashimo ya kuzihifadhia zimemalizia.
Wakati wa hatua ya mtaji duru inaanza kutoka shimo mojawapo la mstari wa nje au wa ndani.
Shimo hilo lazima liwe na kete zaidi na moja (taz. kanuni ya kusambaza) lakini chini ya 16.
Mwisho wa kusambaza lazima iwezekane kula (kula ni lazima).
Mfano:
Mchezaji wa Kusini anaweza kucheza shimo lenye kete 9 tu kuelekea kulia kwa sababu atakula kete 6 zilizomo ndani ya shimo la mpinzani.
Kama kete zilizokula zilikuwamo ndani ya shimo mojawapo la mashimo manne ya katikati zitasambazwa kuanzia kichwa cha kulia kama mwelekeo ulikuwa kinyume na mwendo wa saa, zitasambazwa kuanzia kichwa cha kushoto kama mwelekeo ulikuwa na mwendo wa saa.
Kama haiwezekani kula, mchezaji lazima atakate.
Kama haiwezekani kutakata kuanzia mstari wa ndani, mchezaji anaruhuziwa kutakata kuanzia mstari wa nje.
Kama nyumba bado inamilikiwa na mchezaji, itabaki mali yake mpaka italiwa mara ya kwanza.
Wakati wa hatua hii kanuni za kunamua za nyumba hazina nguvu tena, hairuhuwi kutakatiwa.
Kama mchezaji analazimishwa kutakata, lakini anaweza kucheza ili:
mpinzani haruhusiwi kuondoa kete kutoka shimo hili linatakatiwa.
Mfano:
Mchezaji wa Kusini ametakata ili baadaye aweze kula kete 2 zilizomo ndani ya shimo la mpinzani, kwa hiyo mchezaji wa Kaskazini anaruhusiwa kucheza mashimo yenye kete 10 tu.
Lakini, shimo hili:
Mfano:
Mchezaji ametakata ili baadaye aweze kula kete 10 zilizomo ndani ya shimo la mpinzani, lakini hakutakatia, kwa sababu shimo hilo tu la mstari wa ndani wa mpinzani wake lina kete zaidi ya moja.