Kwa matumizi tofauti ya jina hili tazama Atlas (maana)
Atlasi ni mkusanyiko wa ramani zinazounganishwa pamoja kwa umbo la kitabu. Siku hizi zinapatikana pia kwa umbo la elektroniki kwa matumizi ya kompyuta au kwenye intaneti.
Kwa kawaida atlasi hua na ramani mbalimbali za nchi, bara au Dunia yote. Kuna pia atlasi za anga zinazoonyesha nyota. Neno linatumiwa pia kwa mkusanyiko wa michoro ya anatomia ikionyesha mifupa au viungo vya mwili.
Atlasi huonyesha ramani za aina tofautitofauti kama tabia za kijiografia, kisiasa au kiuchumi.