Utukufu wa mtoto Kristo mbele ya Mungu Baba na Roho Mtakatifu. Sehemu ya mchoro wa Daniel Gran Vienna, Austria. Adamu na Eva wamechorwa chini wamefungwa minyororo.
Yesu akiwatoa Adamu na Eva nje ya makaburi yao siku ya kiyama, Istanbul, Uturuki.

Adamu mpya, Adamu wa pili au Adamu wa mwisho (1Kor 15:45) ni kati ya majina ya Yesu katika Agano Jipya.[1][2][3]

Humo mara mbili Mtume Paulo anafananisha Yesu na Adamu.

Katika 1Kor 15:22 anasema, "kama vile katika Adamu wote wanakufa, vivyo hivyo katika Kristo wote watafanywa hai" na katika mstari wa 45 unamuita Yesu "Adamu wa mwisho".

Halafu katika Rom 5:12–21 anasema, "kama vile kwa kosa la mtu mmoja wengi wamefanywa wakosefu, vivyo hivyo kwa utiifu wa mmoja wengi watafanywa waadilifu" (Rom 5:19).

Katika teolojia

[hariri | hariri chanzo]

Kutokana na Yesu kuitwa Adamu mpya, Bikira Maria alifananishwa na Eva kuanzia karne ya 2 (Irenei), kwa jinsi alivyoshirikiana naye kama Eva mpya.

Katika Kurani

[hariri | hariri chanzo]

Quran pia inafananisha Yesu na Adamu kwa jinsi walioumbwa[4].

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi

[hariri | hariri chanzo]
  1. Watson E. Mills, Roger Aubrey Bullard, eds, Mercer dictionary of the Bible. 1998, p. 10. ISBN 0-86554-373-9
  2. James D. G. Dunn, The Theology of Paul the Apostle. 2006, p. 241 [1]. ISBN 0802844235
  3. John MacArthur, Matthew 1–7, Volume 1. 1985, p. 132. ISBN 0802407552
  4. Sura Al-Imran says, "Verily, the likeness of Jesus before Allah is the likeness of Adam. He created him from dust, then He said to him: 'Be!' – and he was." http://kaheel7.com/eng/index.php/numeric-miracle/137-amazing-miracle-jesus-and-adam

Marejeo

[hariri | hariri chanzo]
Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Adamu mpya kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.