Mahali pa Wafaranki katika karne ya 3.
Kazi bora ya usanii majengo wa Kikarolo: kanisa palatina huko Aachen, Ujerumani.
Milki ya Wafranki wakati wa kifo cha Karolo Mkuu mnamo mwaka 814.

Wafaranki walikuwa Wagermanik waliovamia Dola la Roma na hatimaye kujitokeza kama kabila lenye nguvu kuliko yote ya aina hiyo.

Nchi ya Ufaransa imepata jina lake kutoka kwao, ambao waliitawala na kutoka huko wakaeneza himaya yao juu ya sehemu kubwa ya Ulaya Magharibi, wakizuia Waislamu wasiweze kutoka Hispania.

Ushirikiano wao na Mapapa, kama kabila la kwanza la Kijerumani kuingia Kanisa Katoliki bila kupitia kwanza Uario, ni kati ya mambo yaliyoathiri zaidi historia ya Ulaya.

Kilele cha ustawi wao kilifikiwa chini ya mfalme Karolo Mkuu aliyetawala sehemu kubwa za Ufaransa, Ujerumani, Italia ya kaskazini pamoja na Ubelgiji na Uholanzi ya leo. Papa Leo III alimpa taji la Kaizari wa Roma tarehe 25 Desemba 800. Ndio mwanzo wa Dola Takatifu la Roma. Baada ya Karolo milki yake iligawiwa pande mbili zilizoendelea tofauti na kuwa asili ya mataifa ya Ufaransa na Ujerumani.

Marejeo

Vyanzo

Marejeo mengine

Viungo vya nje

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Wafaranki
Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Wafaranki kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.