Rupia ni jina la pesa inayotumika leo huko India na katika nchi mbalimbali za Asia.
Ni pia jina la pesa iliyowahi kutumika Afrika ya Mashariki na nchi mbalimbali.
Neno "rupia" limetokana na lugha ya Kihindi cha kale "rūp" au "rūpā" linalomaanisha "fedha". Katika lugha ya Sanskrit "rupyakam" (रूप्यकम्) inamaanisha sarafu ya fedha. Hii ni asili ya "Rūpaya" iliyotumika katika India kama sarafu yenye gramu 11.66 za fedha tangu mwaka 1540. Rupia moja ilikuwa na Anna 16, Paisa 64 au Pai 192.
Leo hii nchi zifuatazo zinatumia jina la Rupia (Rupiah, Rupee: ₨) kwa pesa zao:
Rupia ilikuwa pesa ya nchi na maeneo yafuatayo: