Rukuba ya Rami (Alfa Sagittarii, Rukbat)
Rukuba ya Rami (Rukbat) katika kundinyota lake la Kausi (Sagittarius)
Kundinyota Kausi (Mshale) (Sagittarius)
Mwangaza unaonekana 3.97[1]
Kundi la spektra B8 V
Paralaksi (mas) 30.49
Umbali (miakanuru) 182
Mwangaza halisi +0.23
Masi M☉ 2.95
Nusukipenyo R☉ 2.49
Mng’aro L☉ 117
Jotoridi usoni wa nyota (K) 12387
Majina mbadala CD−40° 13245, FK5 728, GC 26737, HD 181869, HIP 95347, HR 7348, SAO 325060, PPM 353699


Rukuba ya Rami (lat. & ing. Rukbat, pia α Alfa Sagittarii, kifupi Alfa Sgr, α Sgr) ni kati ya nyota angavu kwenye kundinyota la Kausi (Mshale) (Sagittarius).

Jina

[hariri | hariri chanzo]

Nyota ya Rukuba ya Rami inayomaanisha “goti la mpiga mishale” ilijulikana kwa mabaharia Waswahili tangu miaka mingi wakifuata njia yao baharini wakati wa usiku kwa msaada wa nyota. [2]. Walipokea jina hili kutoka kwa Waarabu wanaoijua kama ركبة الرامي rukba ar-rami wakitafsiri maelezo katika Almagesti “kwenye goti la mguu wa kushoto”. [3].

Kwa matumizi ya kimataifa Umoja wa Kimataifa wa Astronomia ulikubali jina la Kiarabu na kuorodhesha nyota hii kwa tahajia ya "Rukbat" [4].

Alfa Sagittarii ni jina la Bayer ikiwa ni nyota angavu ya 16 katika Kausi ingawa Alfa ni herufi ya kwanza katika Alfabeti ya Kigiriki. Hii ni mfano jinsi gani Bayer hakufuata mwangaza kikamilifu wakati wa kugawa majina ndani ya kundinyota.

Tabia

[hariri | hariri chanzo]

Rukuba ya Rami ni nyota yenye rangi ya buluu maana ina jotoridi kubwa. Nyuzi za Kelvini 12300 zinaendana pamoja na mng’aro wake ulio zaidi ya mara 100 wa ule wa Jua letu ingawa masi yake ni mara tatu ya Jua tu.

Utafiti wa spektra yake unaonyesha ya kwamba nyota hii inazungukwa na wingu la vumbi na mara nyingi mawingu ya aina hii ni asili ya sayari ingawa hadi sasa hakuna sayari iliyotambuliwa. Spektra inaonyesha vilevile dalili za kuwa na nyota msindikizaji lakini pia hii haikuthibitishwa bado.

Tanbihi

[hariri | hariri chanzo]
  1. Vipimo kufuatana na Docobo et al. (2007)
  2. ling. Knappert 1993
  3. Allen, Star-Names (1899), uk. 357, Tooner, Almagest ,uk. 374
  4. Naming Stars, tovuti ya Umoja wa Kimataifa wa Astronomia (Ukia), iliangaliwa Novemba 2017

Viungo vya Nje

[hariri | hariri chanzo]


Marejeo

[hariri | hariri chanzo]