Ngamia wa Asia yuko katika kanda inayoanzia Anatolia hadi Manchuriakaskazini mwa China. Amezoea zaidi baridi ya Asia ya Kati; wakati wa majira barafu halijoto ya mazingira inafikia -30°C. Joto kali inampa matatizo kidogo na kumchelewesha.
Umbile lao limelingana na mazingira ya jangwani. Miguu ni mipana na kuzuia wasizame chini kwenye mchanga. Nywele ni ndefu, hivyo zinakinga dhidi ya joto na baridi.
Nundu ni mahali pa stoo ya akiba ya mafuta; kama ngamia anapitia mahali pasipo chakula anatumia mafuta kwa nishati ya mwilini. Hahitaji kula kwa kipindi hadi siku 30.
Wanaweza kushika lita 100–150 mwilini na kuendelea jangwani bila kunywa maji kwa wiki mbili. Penye majani mabichi ya kutosha, na kama joto si kali mno, ngamia anaweza kuendelea bila kunywa kwa wiki kadhaa.
Shingo ni ndefu kwa sababu kwa chakula anapendelea majani ya miti na vichaka.
Maisha
Ngamia wa Asia (C. bactrianus) ana nundu mbili
Ngamia ni wanyama wa kijamii na kwa asili huishi katika makundi ya dume mmoja na majike kadhaa. Siku hizi kuna ngamia wa Asia mamia kadhaa kwenye pori ambao ni mabaki ya ngamia pori wa zamani. Wako China na Mongolia.
Ngamia nundu-moja si wanyama wa pori asilia tena; inaaminiwa walitokea Uarabuni. Lakini kuna wanyama waliotoroka huko Australia na Amerika wanaoishi peke yao, hawafugwi.
Ngamia na binadamu
Binadamu akiongozana na ngamia
Ngamia wamefugwa na binadamu tangu miaka 5,000–6,000 iliyopita. Leo hii mifugo hao ni takriban milioni 19 na idadi kubwa, yaani milioni 14, wako Afrika, milioni 7 pekee nchini Somalia na milioni 3.3 nchini Sudan.
Watu hufuga ngamia kwa kubeba watu na mizigo. Nywele zao ni aina ya sufu inayotumiwa kutengenezea mashuka, mahema na pia vitambaa vya nguo. Wanachinjwa kwa nyama yao.
Ngamia hukamuliwa pia kama ng'ombe. Katika nchi yabisi kiasi cha maziwa yao yanalingana na ya ng'ombe.
Katika miaka ya nyuma Wamasai wa Kenya na pia Tanzania wameanza kufuga ngamia baada ya kuona ya kwamba ng'ombe zao walikufa wakati wa ukame lakini ngamia waliendelea kuishi na kutoa maziwa.
Ngamia anachukua chakula chake kwenye mti wenye mizizi mirefu kushinda manyasi yanayoliwa na ng'ombe. Kwa sababu hiyo manyasi hukauka haraka wakati wa ukame kuliko majani ya miti.
Katika Biblia
Katika mazingira ambako Biblia iliandikwa, ngamia alikuwa mnyama mkubwa kuliko wote wa nchi kavu. Ndiyo sababu alitumika katika methali mbalimbali kwa kusisitiza jambo.
Kwa mfano, Yesu alisema, "Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu la sindano kuliko tajiri kuingia mbinguni" (Mk 10:23-27).
Picha
Ngamia nundu-moja sokoni huko Nouakchott, Mauritania
Wilson, R.T. (1984). The camel. New York: Longman. ISBN 0-582-77512-4.
Yagil, R. (1982). Camels and Camel Milk. FAO Animal Production and Health Paper. Juz. 26. Rome: Food And Agriculture Organization Of The United Nations. ISBN 92-5-101169-9. ISSN 0254-6019.
Gilchrist, W. (1851). A Practical Treatise on the Treatment of the Diseases of the Elephant, Camel & Horned Cattle: with instructions for improving their efficiency; also, a description of the medicines used in the treatment of their diseases; and a general outline of their anatomy'. Calcutta: Military Orphan Press.
Indian Spotted Chevrotain (M. indica) · Yellow-striped Chevrotain (M. kathygre) · Sri Lankan Spotted Chevrotain (M. meminna)
Tragulus
Java Mouse-deer (T. javanicus) · Lesser Mouse-deer (T. kanchil) · Greater Mouse-deer (T. napu) · Philippine Mouse-deer (T. nigricans) · Vietnam Mouse-deer (T. versicolor) · Williamson's Mouse-deer (T. williamsoni)
Kuro (K. ellipsiprymnus) ·Mraye (K. kob) · Lechwe kusi (K. leche) · Lechwe wa Nili (K. megaceros) · Lechwe wa Upemba (K. anselli) ·Sheshe (K. vardonii)
Swala wa Cuvier (G. cuvieri) · Swala-jangwa (G. dorcas) · Swala mhindi (G. bennettii) · Swala-milima (G. gazella) · · Swala mwajemi (G. subgutturosa)Swala wa Neumann (G. erlangeri) · Swala wa Sahara (G. leptoceros) · Swala wa Saudia (G. saudiya) · Swala wa Speke (G. spekei)
Palawan Bearded Pig (S. ahoenobarbus) · Bearded Pig (S. barbatus) · Indo-chinese Warty Pig (S. bucculentus) · Visayan Warty Pig (S. cebifrons) · Celebes Warty Pig (S. celebensis) · Flores Warty Pig (S. heureni) · Oliver's Warty Pig (S. oliveri) · Philippine Warty Pig (S. philippensis) · Nguruwe-mwitu wa Ulaya (S. scrofa) · Timor Warty Pig (S. timoriensis) · Javan Pig (S. verrucosus)