Mtaala wa kwanza kuchapwa (1576).

Mtaala (kutoka Kiarabu; kwa Kiingereza curriculum) ni mpangilio wa mambo ambayo mwanafunzi anatarajiwa kusaidiwa kujua hatua kwa hatua.

Mtaala unaweza kupanga hata ushirikiano unaotarajiwa kati ya mwalimu na wanafunzi wake ili kufikia shabaha za shule au chuo.

Nchi nyingi zina mitaala iliyopangwa kikamilifu kwa ngazi zote za elimu.

Baadhi inamuachia mwalimu nafasi kubwa zaidi ya kuona mwenyewe la kufundisha kadiri ya mahitaji ya wanafunzi wake.

Ofisi ya Kimataifa ya Elimu chini ya UNESCO ndiyo yenye jukumu hasa la kupitia mitaala na utekelezaji wake duniani kote.

Mtaala na falsafa ya nchi

Mitaala ni jumla ya mipango na uzoefu ulioratibiwa kwa ajili ya mafunzo ya aina fulani yenye malengo maalumu kwa wanafunzi. Mipango hiyo inaweza kuwa ni mambo, matendo na uzoefu wa aina yoyote ile ambayo wanafunzi wanapata chini ya uongozi na usimamizi wa shule. Hutegemea falsafa ya nchi na siasa inayoiongoza.

Mfano: nchini Tanzania falsafa ya nchi ni: Ujamaa na Kujitegemea (kutokana na siasa iliyokuwa ikiongoza chini ya Mwalimu Julius K. Nyerere. Falsafa ya elimu ni: Elimu ya Kujitegemea (inatokana na falsafa ya nchi). Madhumuni/Malengo Makuu ya Elimu nchini yameanishwa katika Sera ya Elimu ya Taifa na katika mihtasari ya masomokwa kila ngazi (Awali, Msingi, Sekondari na Elimu ya Juu)

Bila mwongozo wa falsafa ya nchi na madhumuni ya elimu kitaifa wakuza mitaala watakosa mwelekeo maalumu wa ukuzaji mitaala. Hivyo ina hatari ya kufanya mtaala uwe mkusanyiko wa mambo yasiyokuwa na mwelekeo maalumu kitaifa. Madhara yake ni watumiaji kukosa mwelekeo na msimamo maalumu unaolingana na mwelekeo wa kitaifa.

Sifa za mtaala

Kwa hiyo mtaala ni jumla ya mpango uliondaliwa kwa ajili ya kufundishia na kujifunza kwa lengo la kuwapatia walegwa maarifa ,stadi na mielekeo mbalimbali. Nguzo kuu ya mtaala ni muhtasari ambayo hutumika katika kutekeleza mtaala huo.

Muhtasari: Ni mkusanyiko wa mada zinazokusudiwa ili kukamilisha kiwango fulani cha elimu , kazi au mafunzo maalumu.Katika shughuri za wakuza ukuzaji mitaala, wakuza mitaala wanapaswa kuongozwa na malengo makuu ya elimu yanayowekwa kitaifa.

Umuhimu wa kuwa na mtaala

Matumizi ya mtaala

Aina za mitaala

  1. Mtaala rasmi
  2. Mtaala usiyo rasmi
  3. Mtaala ficho

Mtaala rasmi

Ni mkusanyo wa mambo yote anayopaswa kuyafanya na kuyafahamu mwanafunzi anapokuwa darasani. Au ni mtaala uliopangwa kwa madhumuni ya kumfundisha mwanafunzi katika mfumo rasmi wa elimu.

Sifa za mtaala rasmi

Faida za mtaala rasmi

Mapungufu ya mtaala rasmi

Mitaala isiyo rasmi

Ni mtaala unaofundisha mambo yote anayopaswa kujifunza mtoto nje ya mtaala ulio rasmi katika maisha ya kawaida ya kujifunzia. Mara nyingine mtaala huu huitwa mtaala uliofichika.

Mara nyingi mitaala hiyo huandaliwa kulingana na mahitaji ya jamii ya mwanafunzi na jamii husika kwa wakati ule.

Sifa za mtaala usio rasmi

Mapungufu

Mtaala ficho

Mtaala huu unajumuisha matendo yote yanayosaidia ujifunzaji usiokusudiwa au usioratibiwa. Kwa mfano ujifunzaji wa utii kwa mamlaka, kuwahi/kujali muda, usafiri nakadhalika. Yaani unajumuisha mambo yote ambayo hayaonekani kwenye muhtasari wa shule kama sehemu ya mtaala.

Vipengele vya mtaala

Katika mtaala vipengele vilivyo muhimu ni vitano ambavyo hufanya kazi kwa ushirikiano na kwa kutegemeana:

  1. Malengo ya mtaala
  2. Maudhui
  3. Njia za kufundishia
  4. Zana
  5. Tathmini

Vipengele hivi vitano hufanya kazi kwa ushirikiano na kwa kutegemeana kama viungo vya mwili wa binadamu. Ni vigumu kuvitenganisha ila kwa faida ya kujifunza na kuelewa kwa undani, tutavitazama kimoja kimoja katika maelezo.

Malengo ya mtaala

Malengo ni matokeo au matarajio yanayotarajiwa kupatikana kutokana na mpango/programu fulani. Mtaala wowote ule lazima uwe na malengo. Katika uwanja wa elimu, malengo ya mtaala ni mabadiliko ya tabia na mwenendo wyanayotarajiwa kupatikana kwa wanafunzi baada ya kupata programu fulani ya mafunzo.

Umuhimu wa malengo ya mtaala

Malengo kama kipengele cha msingi cha mtaala yana umuhimu mkubwa kwani:

Malengo ya jumla na malengo mahususi

Malengo ya jumla ni matarajio au mabadiliko kitabia ambayo tunatarajia kuyaona kwa mtu ambae amepata elimu.Malengo ya jumla ni malengo na madhumuni ya elimu kitaifa yaliyokusudiwakutimizwa na program mbalimbaliza mafunzokatika viwango mbalimbali vya elimu. Kimsingi malengo haya yanatokana na sera ya elimu katika nchi husika.

Baadhi ya malengo ya kitaifa ni

Sifa za malengo ya jumla

Malengo mahususi

Malengo mahususi ya mtaala hutokana na malengo ya jumla. Haya ni malengo yaliyokusudiwa kutimizwa na programu mbalimbali za mafunzo katika viwango mbalimbali vya elimu.

Ni kutokana na malengo mahususi kila kiwango cha ngazi fulani ya elimu ndiyo yanapatikana mahususi yanayowaongoza walimu katika kuandaa maazimio yao wanayofundishia darasani.

Maudhui haya ndio yawezayo kumuongoza mwalimu kutoa maarifa na stadi ambazo zinaweza kubadili tabia ya mwanafunzi ambayo inaweza kupimika.

Kwa mfano tunapofundisha somo la Hisabati,tunatarajia kuona mabadiliko fulani katika tabia ya mtoto kutokana na kujifunza somo zima au mada fulani. Mabadiliko hayo yanaweza yakawa maarifa,stadi au mwelekeo mwanafunzi anaouonyesha kutokana na kujifunza somo la Hisabati ambao hakuwa nao kabla ya kujifunza somo hilo.

Tunaweza kugawa malengo mahususi katika Nyanja tatu ambazo ni

Sifa za malengo mahususi

Maudhui

Katika kuunda maudhui ya mtaala ni vizuri kuzingatia maswali kama vile:

Misingi/vigezo vya kuchagua maudhui ya mtaala

Njia na mbinu

Ili kuweza kufanikisha tando zima la ufundishaji katika kufanikisha maudhui na malengo ya somo mwalimu hutumia vitendo mbalimbali vijulikanavyo kama njia. Na njia peke yake haiwezikufanikisha somo lazima isaidiwe na mbinu. Mbinu ni stadi maalumu inayobainisha ni jinsi gani ya kufundishia/kujifunzia itakvyowezeshwa katika tendo la kufundisha na kujifunza. Njia ni namna mwalimu anavyowasilisha mada katika mchakato mzima wa kufundisha.

Kuna njia mbili zinazoweza kutumika katika swala zima la kujifunzia na kujifunza:

  1. Njia shirikishi
  2. Njia isiyo shirikishi

Misingi ya kuchagua njia/mbinu

Vifaa vya mtaala

Mtaala una vifaa vyake maalumu ambavyo vinatakiwa vitumike kwa usahihi ili kutekeleza mtaala kwa ufanisi. Vifaa hivyo ni:

Muhtasari

Muhtasari ni mwongozo unaotaja kwa kifupi tu mambo yote yanayotakiwa yafundishwe katika mwaka mzima katika darasa fukani au kwa miaka kadhaa kwa kila darasa kwa mmpangilio maalumu.

Muundo wa muhtasari

Muhtasari una sehemu kuu mbili:

  1. Utangulizi: Hii ni sehemu ambayohuelekeza sababu za kuwepo kwa muhtasari huo, muundo wake , malengo ya elimu katika kiwango husika na malengo ya kufundisha somo hilo katika kiwango hicho.
  2. Majedwali ya kutumia kufundishia: Hii ni sehemu ambayo huwa na maudhui ya somo husika yanayotakiwa kufundishwa kila mwaka. Majedwali ya kufundishia yana vipengele vikuu vilivyopangwa katika safukama ifuatavyo.

Vipengele vya muhtasari

  1. Mada kuu na mada ndogo
  2. Lengo la kufundishia mada hiyo
  3. Mapendekezo ya njia za kufundishia na kujifunzia
  4. Vifaa /zana za kujifunzia na kufundishia

Matumizi ya muhtasari

Kitabu cha kiada

Ni kitabu ambacho kinafafanua mada zote za muhtasari kwa ukamilifu. Kitabu hiki ndicho kinachobeba maudhui ya somo kwa ukamilifu.Mfano vitabu malimbali vya masomo vilivyomo mashuleni.

Sifa za kitabu cha kiada

Matumizi ya kitabu cha kiada

Mwalimu hukitumia kwa kuelekeza maarifa. Hutumiwa na mwanafunzi pia kwa kujikumbushia na kufanya marudio.

Uchambuzi wa kitabu cha kiada

Vitabu vingi vya kiada vimeandaliwa katika mitindo tofautitofauti, hivyo ni jukumu la mwalimu w somo pengine akishirikiana na wanafunzi kuchagua kitabu kinachofaa. Ili kuweza kufanya uamuzi wa kitabu kinachofaa huna budi kuchambua kwa kuzingatia mambo yafuatayo: Kwa kiasi gani mada zote za muhtasari zimefafanuliwa kwa ufanisi pamoja na kuzingatia sifa za kitabu cha kiada.

Kiongozi cha mwalimu

Hiki ni kitabu kinachompa mwalimu maelekezo ya mada ya kufundisha, jinsi ya kuifundisha, maudhui gani yafundishwe na kutumia vifaa au zana gani. Pia kinaitwa kitabu cha mwongozo kwa mwalimu.

Sifa za kiongozi cha mwalimu

Umuhimu wa kitabu cha mwalimu

Dhana ya kitabu cha mwalimu

Sifa za kitabu cha mwalimu

Tofauti kati ya kitabu cha mwalimu na kiongozi cha mwalimu

Vyanzo vya mitaala

Ni muhimu kujua vyanzo vya mtaala ili kuhakikisha vinahusishwa na kuzingatiwa wakati wa kuandaa mtaala. Vyanzo hivyo ni pamoja na

Marejeo

Wizara ya elimu na Utamaduni(2005).mpango wa mafunzo ya walimu kazini Daraja la IIIC/B-A: Moduli ya soma la Mitaala. Wizara ya elimu na Utamaduni.

Makala hii kuhusu mambo ya elimu bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mtaala kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.