Konyeza
Konyeza madoa (Mastigias papua)
Konyeza madoa (Mastigias papua)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia
Nusuhimaya: Eumetazoa
Faila: Cnidaria (Wanyama-upupu)
Nusufaila: Medusozoa (Konyeza)
Ngazi za chini

Ngeli 4:

  • Cubozoa (konyeza-sanduku) Werner, 1973
  • Hydrozoa (konyeza wadogo) Owen, 1843
  • Scyphozoa (konyeza sahihi) Götte, 1887
  • Staurozoa (konyeza-kikonyo) Marques & Collins, 2004

Konyeza ni wanyama wa bahari au wa maji baridi. Wanaainishwa katika nusufaila Medusozoa wa faila Cnidaria (wanyama-upupu). Wana minyiri mirefu au mifupi yenye seli zinazochoma ngozi na zinazoweza kupooza au hata kuua mawinda madogo. Hutumika kwa kukamata samaki wadogo na wanyama wengine wa bahari.

Kwa kawaida konyeza ni wanyama wa bahari ambao huogelea vihuru. Mwili wao ni kama kuba lenye umbo la bakuli na chini yake kuna minyiri inayojiburura nyuma. Konyeza kama hao huitwa medusa pia kwa Kiingereza, ingawa wachache wametiwa nanga kwa kikonyo kwenye sakafu ya bahari badala ya kuwa sabili. Kuba linaweza kudundadunda ili kujisukuma na kuogelea kwa ufanisi. Konyeza wana mzunguko tata wa maisha. Medusa kwa kawaida ni awamu ya kijinsia, ambayo hutoa lava wa planula wanaotawanyika sana na kuingia katika awamu ya chechevule (isiyo na jinsia) ambayo inakaa mahali pamoja mpaka kufikia ukomavu wa kijinsia.

Konyeza hupatikana duniani kote, kutoka maji ya juu hadi kwenye kina kirefu cha bahari. Scyphozoa ("konyeza sahihi") hutokea baharini tu, lakini baadhi ya Hydrozoa wenye muonekano kama hao huishi katika maji baridi. Konyeza wakubwa, wenye rangirangi mara nyingi, wapo kwa kawaida katika maeneo ya pwani duniani kote. Medusa za spishi nyingi hukua haraka na hukomaa ndani ya miezi michache kisha hufa mara tu baada ya kuzaliana. Kinyume chake, awamu ya chechevule, iliyoshikamana na sakafu ya bahari, inaweza kuishi muda mrefu zaidi. Konyeza wamekuwepo kwa angalau miaka milioni 500, na labda miaka milioni 700 au zaidi, ambayo inawafanya kuwa kikundi cha wanyama wa ogani nyingi cha zamani zaidi.

Ngeli

Picha