Sefania akiwahubiria watu (mchoro wa huko Ufaransa, karne ya 16.

Kitabu cha Sefania ni kimojawapo kati ya vitabu vya Tanakh (yaani Biblia ya Kiebrania), hivyo kinapatikana pia katika Agano la Kale ambalo ni sehemu ya kwanza ya Biblia ya Kikristo.

Kutokana na ufupi wake kimepangwa tangu kale kati ya vitabu 12 vya Manabii Wadogo.

Mhusika

Nabii Sefania, mtu wa Yerusalemu alihubiri kwa nguvu (640-625 hivi K.K.) mwanzoni mwa utawala wa mfalme Yosia, kabla huyo hajaanza urekebisho wake wa kidini uliofuata kuvumbua katika hekaluni maandiko ya Kumbukumbu la Sheria.

Ujumbe

Pamoja na kutisha kwa matabiri yake, aliahidi wokovu kwa mabaki ya Israeli, akisema watakuwa watu maskini na walioonewa (3:9-20).

Ndio mwanzo wa imani ya kuwa wapenzi wa Mungu ni hasa mafukara, atakavyosisitiza Yesu (Lk 6:20-21).

Ufafanuzi

Kama vitabu vingine vyote vya Biblia, hiki pia kinatakiwa kisomwe katika mfululizo wa historia ya wokovu ili kukielewa kadiri ya maendeleo ya ufunuo wa Mungu kwa binadamu.

Marejeo

Viungo vya nje

Vitabu vya Agano la Kale

Mwanzo * Kutoka * Walawi * Hesabu * Kumbukumbu * Yoshua * Waamuzi * Ruthu * Samueli I * Samueli II * Wafalme I * Wafalme II * Mambo ya Nyakati I * Mambo ya Nyakati II * Ezra * Nehemia * TobitiDK * YudithiDK * Esta * Wamakabayo IDK * Wamakabayo IIDK * Yobu * Zaburi * Methali * Mhubiri * Hekima DK * SiraDK * Wimbo Bora * Isaya * Yeremia * Maombolezo * BarukuDK * Ezekieli * Danieli * Hosea * Yoeli * Amosi * Obadia * Yona * Mika * Nahumu * Habakuki * Sefania * Hagai * Zekaria * Malaki

Alama ya DK inaonyesha vitabu vya deuterokanoni visivyopatikana katika matoleo yote ya Biblia.

Makala hii kuhusu mambo ya Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kitabu cha Sefania kama historia yake au athari wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.