Kieuskara (au Kibaski) ni lugha hai ya pekee[1] inayotumiwa na Wabaski hasa mpakani mwa Hispania kaskazini na Ufaransa kusini-magharibi kwenye milima ya Pirenei karibu na bahari ya Atlantiki.[2]
Ingawa inakubalika ilikuwa inatumika huko kabla ya lugha za Kihindi-Kiulaya kuenea Ulaya magharibi, haieleweki ilianzaje, kwa sababu hakuna lugha yoyote inayofanana nayo.
Wanaoitumia ni kama watu 715,000, wengi wao wakiwa Hispania, ambako inalindwa na kustawishwa zaidi.
Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Kieuskara kama historia yake, uenezi au maendeleo yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |