Dk. Joyce Cherono Laboso ni mwanasiasa wa Kenya na mbunge katika bunge la Kenya
Yeye anawakilisha Jimbo la uchaguzi la Sotik katika bunge la Kumi. Alikichukua kiti hiki kutoka kwa dadake Lorna Laboso ambaye alifariki katika ajali ya ndege mnamo 10 Juni 2008.
Katika Uchaguzi mdogo uliofanyika 25 Septemba 2008, Dk. Laboso aliyekuwa akiwania kiti hicho kwa tiketi ya ODM, aliwabwaga wapinzani wengine 11 na kujinyakulia kura 23,880; ushindi wa zaidi ya kura 10,000 kuliko mpinzani wake wa karibu Alexander Sitienei aliyezoa kura 13,843.
Kabla ya kuchaguliwa kuwa mbunge, Dk. Laboso alikuwa mkufunzi wa lugha ya Kifaransa katika Chuo Kikuu cha Egerton.
Sasa hivi ni mwanakamati katika Kamati ya Kitaifa ya Jinsia na Maendeleo.
Makala hii kuhusu mwanasiasa huyo wa Kenya bado ni mbegu. Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |